
Man United wapo kwao Old Trafford huku Wiki iliyopita huko Denmark, wakichapwa 2-1 na FC Midtjylland, na hivyo Leo ni ushindi tu ndio utawakomboa.
Huko Anfield, Liverpool wanatinga kurudiana na Augsburg ya Germany ambayo walitoka nayo 0-0 huko Germany Wiki iliyopita na hivyo ushindi au Sare yeyote ya Magoli ni faida kwao.
Nako huko White Hart Lane Jijini London, Wenyeji Tottenham Hotspur watacheza na Fiorentina ya Italy ambayo walitoka nayo 1-1 na sasa ushindi au Sare ya 0-0 itawafaa Spurs.

Lakini Sare yeyote ya kuanzia 2-2 kwenda juu itawatupa nje Spurs.