
Mourinho amekuwa hana kibarua tangu atimuliwe Chelsea Mwezi Desemba lakini amekuwa akihusishwa sana na kumrithi Louis va Gaal huko Man United.
Kwa mujibu wa Gazeti la Spain, El Pais, chanzo kutoka kwa Wakala wa Mourinho, Kampuni ya Jorge Mendes, imethibitisha kuwa Mreno huyo mwenye Miaka 53 alisaini Mkataba wa awali na Man United tangu Mwezi uliopita.


