
Kijana huyo wa Miaka 19 hatakaa City kwa Msimu huu unaokuja wa 2016/17 na badala yake atapelekwa huko Spain kucheza kwa Mkopo kwenye Klabu ya Deportivo La Coruna.
Moreno anakuwa Mchezaji wa 3 kusainiwa na Meneja mpya wa City Pep Guardiola Wiki hii baada ya pia kuwasaini Winga Leroy Sane toka Schalke ya Germany na Fowadi Gabriel Jesus wa Palmeiras ya Brazil.
